Papa Sixtus II

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Sixtus II
Remove ads

Papa Sixtus II alikuwa Papa kuanzia tarehe 30 Agosti 257 hadi kifodini chake tarehe 6 Agosti 258[1]. Alitokea Ugiriki[2].

Thumb
Kuuawa kwa Papa Sixtus II na mashemasi wake 6.

Alimfuata Papa Stefano I akafuatwa na Papa Dionysius.

Alirudisha umoja na makanisa ya Mashariki na Afrika Kaskazini uliowahi kuhatarishwa na misimamo tofauti kuhusu ubatizo uliotolewa na waliojitenga na Kanisa Katoliki.

Alikamatwa akihubiria ndugu wa imani juu ya sheria za Mungu wakati wa adhimisho la ekaristi[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini pamoja na mashemasi wake sita: Januari, Vinsenti, Magnus, Stefano, mbali ya Agapito na Felisisimi waliouawa siku hiyohiyo sehemu nyingine chini ya kaisari Valeriani[4]. Katika Kanuni ya Kirumi anatajwa pamoja na shemasi wake wa saba, Laurenti, aliyeuawa siku tatu baadaye.

Sikukuu yake ni tarehe 7 Agosti[5].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads