Papa Celestino V

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Celestino V
Remove ads

Papa Celestino V, O.S.B. (121519 Mei 1296) alikuwa Papa kuanzia tarehe 5 Julai/29 Agosti 1294 hadi 13 Desemba 1294[1]. Alitokea Molise, Italia[2].

Thumb
Mt. Selestini V.

Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Pietro Angelerio wa Morrone. Baada yake hakuna tena Papa aliyejichagulia jina la Celestino.

Alimfuata Papa Nikolasi IV baada ya miaka miwili ya pengo[3], akichaguliwa kutokana na umri wake mkubwa na sifa ya utakatifu na utendaji miujiza [4].

Ni maarufu kwa kuwa mwaka uleule alijiuzulu[5] kwa kujitambua hawezi Upapa [6] ili arudi kuishi maisha ya upwekeni kama mmonaki (mwaka 1244 alikuwa ameanzisha shirika la Waselestini, tawi la Wabenedikto)[7]. Lakini Papa Bonifasi VIII aliyemfuata alimfunga akafuta karibu maamuzi yake yote.

Alitangazwa na Papa Klementi V kuwa mtakatifu tarehe 5 Mei 1313[8].

Sikukuu yake ni tarehe 19 Mei[9].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads