Papa Silverio

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Silverio
Remove ads

Papa Silverio alikuwa Papa kuanzia tarehe 8 Juni 536 hadi mwaka 537[1]. Alitokea Frosinone, Italia[2].

Thumb
Mt. Silveri.

Alimfuata Papa Agapeto I akafuatwa na Papa Vigilio.

Alizaliwa na Papa Hormisdas katika ndoa yake kabla ya kupata upadrisho.

Aliondoshwa madarakani mnamo mwezi Machi 537 kwa nguvu ya Theodora, mke wa Justiniani I, Kaisari wa Bizanti.

Huyo malkia alimpendelea shemasi Vigilio akitarajia ataunga mkono njama zake za kutetea uzushi wa Eutike.

Kumbe Silverio alikataa pia ombi la Theodora la kumrudisha madarakani Antimo kama Patriarki wa Konstantinopoli aliyekuwa ameondolewa na Papa Agapeto I kwa uzushi huohuo [3].

Basi, Silverio alifungwa na kupelekwa uhamishoni katika kisiwa cha Palmarola ambapo alijiuzulu tarehe 11 Novemba 537 akafariki kwa tabu nyingi na njaa tarehe 2 Desemba 537.

Angalau tangu karne ya 11 ameheshimiwa kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Desemba[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads