Papa Silvester I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Silvester I
Remove ads

Papa Silvester I alikuwa Papa kuanzia tarehe 31 Januari 314 hadi kifo chake tarehe 31 Desemba 335[1].

Thumb
Papa Silvesta I na Kaisari Konstantino Mkuu.

Alimfuata Papa Miltiades akafuatwa na Papa Marko.

Mtoto wa Rufinus, mkazi wa Roma, hatuna habari nyingi za maisha yake. Ila ni kwamba aliongoza kwa busara Kanisa Katoliki kwa muda mrefu mara baada ya Kaisari Konstantino Mkuu kulipatia uhuru wa dini na kulijengea maabadi mengi, makubwa tena mazuri.

Wakati wa utawala wake ulifanyika mtaguso mkuu wa kwanza (Nisea, leo nchini Uturuki, 325) uliomshangilia Kristo kama Mwana wa Mungu. Yeye hakuhudhuria, ila alituma wajumbe wawili akathibitisha maamuzi yaliyofikiwa.

Alizikwa katika katakombu la Prisila [2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads