Papa Stefano I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Stefano I
Remove ads

Papa Stefano I alikuwa Papa kuanzia tarehe 12 Machi 254 hadi kifodini chake tarehe 2 Agosti 257[1][2]. Alitokea Roma, Italia, ingawa aliweza kuwa na asili ya Ugiriki.

Thumb

Alimfuata Papa Lucius I akafuatwa na Papa Sisto II.

Alifundisha kwamba waliobatizwa na madhehebu yaliyojitenga na Kanisa Katoliki wameungana na Kristo moja kwa moja, hivyo hawahitaji wala hawatakiwi kubatizwa tena[3], tofauti na walivyodai baadhi ya maaskofu, hasa wa Afrika Kaskazini. Baadaye msimamo wake ulienea kote katika Kanisa la Kilatini.

Inasimuliwa kwamba aliuawa na maaskari wa Kaisari Valerian wakati wa Misa[4] .

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, pengine mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Agosti [5].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads