Papa Lucius I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Lucius I
Remove ads

Papa Lucius I alikuwa Papa kuanzia Juni au Julai 253 hadi kifo chake tarehe 5 Machi 254[1]. Alitokea Roma, Italia.

Thumb
Papa Lucius I.

Alimfuata Papa Kornelio akafuatwa na Papa Stefano I.

Kwa imani yake kwa Kristo, mara baada ya kuwekwa wakfu alipelekwa uhamishoni, lakini aliwahi kurudishwa, akatoa ushahidi wake kwa kukabili kwa upole na busara matatizo ya wakati wake[2][3].

Sipriani wa Carthago alimsifu [4] kwa kukataa msimamo mkali wa wafuasi wa Novasyano dhidi ya waliowahi kuasi ili kuokoa uhai wao.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, hasa tarehe ya kifo chake[5][6].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads