Rikitrude

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rikitrude
Remove ads

Rikitrude (pia: Rictrude, Rictrudis, Richtrudis, Richrudis; 612 - 12 Mei 688) alikuwa mwanamke wa ukoo maarufu wa Ufaransa Kusini Magharibi ambaye tangu ujanani aliongozwa kiroho na Amando akaolewa na Adalbati I akaishi naye maisha maadilifu sana[1][2] .

Thumb
Sanamu ya Mt. Rikitrude huko Boiry-Sainte-Rictrude.

Baada ya mumewe kuuawa, kwa ushauri wa Amando alijiunga na monasteri ya Marchiennes aliyokuwa ameianzisha, akawa abesi wake[3] na kuongoza vizuri sana mabikira waliowekwa wakfu huko[4].

Anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, sawa na mume wake na watoto wao wote wanne, Klotsinda, Adalsinda, Eusebia wa Douai na Morandi.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 12 Mei[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads