Switbati

From Wikipedia, the free encyclopedia

Switbati
Remove ads

Switbati (pia: Suitbert, Suidbert, Suitbertus, Swithbert, au Swidbert; Northumbria, Uingereza, 647 hivi – Kaiserswerth, karibu na Dusseldorf, Ujerumani, 1 Machi 713) alikuwa mmonaki Mbenedikto wa Uingereza aliyepata umaarufu kwa kwenda umisionari pamoja na Wilibrodi kati ya makabila ya Ulaya Kaskazini.

Thumb
Mt. Switbati alivyochorwa.

Baada ya kupewa daraja ya juu na Wilfrido, alifanya utume huo kama askofu hasa katika Frisia na Westfalia, kati ya Uholanzi na Ujerumani za leo[1].

Mwaka 700 hivi alianzisha monasteri alimofariki.

Anaheshimiwa tangu zamani kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads