Thori
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Thori (thorium) ni elementi ya kimetali yenye alama Th na namba atomia 90.
Thori safi ni metali laini yenye rangi ya kifedha-kijivu; baada ya kukaa hewani inaelekea polepole kuwa nyeusinyeusi.
Iligunduliwa Norwei na kupewa jina lake Uswidi mwaka 1829. Jina la Thori limechukuliwa kutoka mungu wa ngurumu wa Skandivia ya Kale.
Thori ni elementi yenye unururifu dhaifu. Isotopi yake ya 232Th ina nusumaisha ya miaka bilioni 14.05 inayozidi hata umri wa Dunia. Wanajiolojia hukadiria kuwa mbunguo nyuklia wa Thori unachangia sana katika joto lililopo ndani ya Dunia[1].
Inapatikana kiasili katika madini, hasa Uhindi, Marekani na Australia. Akiba zake ni kubwa kushinda urani, kwa hiyo kuna majadiliano kama itafaa kutumiwa kwa tanuri nyuklia baada ya kumaliza akiba za urani[2]. Lakini kuna pia wasiwasi kwa sababu inaonekana si thabiti kama urani katika mchakato wa mwatuko nyuklia, hivyo kuna hofu ya ajali pamoja na hatari ya matumizi ya thori kutoka tanuri kwa ajili ya silaha za nyuklia[3].
Remove ads
Marejeo
Tovuti za Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads