Wasuni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Wasuni ni dhehebu kubwa ndani ya dini ya Uislamu. Takriban asilimia 80 - 90 za Waislamu wote duniani hukadiriwa kuwa Wasuni na wengine 10-20 % huhesabiwa kati ya Washia.

Kibichi: Wasuni wengi; Nyekundu: Washia wengi
Wasuni huitwa kwa Kiarabu ahl ul-sunna (Kiarabu: أهل السنة; "watu wa mapokeo"). Neno Suni hutokana na neno sunna (kwa Kiarabu : سنة ) inayomaanisha mapokeo ya Mtume Muhammad.
Isipokuwa Uajemi, Iraki, Bahrain, Azerbaijan, Yemen, Omani na Lebanoni kundi hilo ni kubwa katika nchi zote penye Waislamu wengi.
Remove ads
Historia
Wasuni hufuata mwelekeo wa Uislamu ulioanzishwa na ukhalifa wa Abu Bakr na kutokubali uongozi wa familia ya Mtume Muhammad kupitia Ali, Hassan na Husain.
Madhehebu ya Wasuni
Kati ya Wasuni kuna madhehebu nne zinazotofautiana kiasi kuhusu mafundisho ya sharia au sheria ya kidini ya Kiislamu. Ndio Wahanafi, Wamaliki, Washafii na Wahanbali. Kwa jumla Wasuni hukubaliana ya kwamba madhehebu haya yote manne ni sawa.
Walimu wengine hasa katika kikundi cha Wawahabi kilichoanzishwa kati ya Wahanbali kimekaza mafundisho yake hadi kuwashtaki wengine kuwa si Waislamu wa kweli.
Remove ads
Viungo vya Nje
- ,
Idara Sirat e Mustaqeem (Hanafi Organization)Pakistan Ilihifadhiwa 11 Desemba 2007 kwenye Wayback Machine.
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads