From Wikipedia, the free encyclopedia
Luanda (kirefu: São Paulo de Luanda: pia Loanda) ni mji mkuu pia mji mkubwa wa Angola ikiwa na wakazi 2,487,484 (katika rundu la jiji 7,805,000) wanaongezeka haraka kutoka ndani na nje ya nchi na ya bara la Afrika.
Mji wa Luanda uko mkoani Luanda, kaskazini ya mdomo wa mto Cuanza mwambaoni pa Atlantiki.
Mji ulianzishwa na Wareno mwaka 1575 BK kwa jina la São Paulo de Luanda. Umekuwa mji mkuu wa Angola tangu mwaka 1627.
Hadi mwaka 1850 Luanda ilikuwa kitovu cha biashara ya watumwa kwenda Brazil.
Wakati wa uhuru mwaka 1975 walowezi wengi Wareno waliondoka mjini. Vita ya wenyewe kwa wenyewe katika Angola kati ya miaka 1974 - 2002 ilileta hasara pia kwa mji mkuu.
Kati ya wakazi, walio wengi kabisa ni Waafrika wa makabila kama vile Waovimbundu, Wakimbundu na Wakongo.
Lugha rasmi ni Kireno lakini lugha nyingi za Kibantu zinatumika pia.
Luanda ni bandari muhimu nchini pia mwanzo wa reli kwenda Malange.
Makala hii kuhusu maeneo ya Angola bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Luanda kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.