Adomnani

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Adomnani (pia: Adomnán, Adamnán, Adamnanus, Adhamhnán, Eunan; Ireland Kaskazini, 624 hivi - Iona, Uskoti, 704 hivi) mmonaki padri aliyeongoza kama abati monasteri ya kisiwa cha Iona huko Uskoti tangu mwaka 679 hivi hadi kifo chake[1].

Thumb
Mt. Adomnani katika dirisha la kioo cha rangi la kanisa kuu la Raphoe.

Mwenye ujuzi mkubwa wa Biblia ya Kikristo na mpenzi wa umoja na amani asiyechoka kuvipigania, kwa mahubiri yake alisaidia wengi katika Ireland na Uskoti vilevile kukubali maamuzi ya Sinodi ya Whitby kuhusu kuadhimisha sherehe ya Pasaka kwa kufuata mapokeo ya Kanisa la Roma badala ya yale ya Ukristo wa Kiselti[2].

Yeye aliandika maisha ya Kolumba[3], jamaa wa baba yake[4], na Beda Mheshimiwa aliandika juu ya Adomnani mwenyewe aliyemfahamu mapema.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana[5] kama mtakatifu.

Sikukuu yao ni tarehe 23 Septemba[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo mengine

Marejeo mengine tena

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads