Alberto wa Pontida
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Alberto wa Pontida, O.S.B., (Prezzate, 1025; 2 Septemba 1095) alikuwa abati huko Lombardia, Italia.
Alberto alikuwa kati ya wamonaki waliojitahidi zaidi kueneza urekebisho wa Cluny katika mkoa huo. Hata hivyo, alikuwa upande wa kaisari Henri IV wa Ujerumani katika mashindano yake na Papa Gregori VII.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 2 Septemba[1] pamoja na mwenzake Vito[2].
Remove ads
Maisha
Kabla hajajiunga na umonaki, alikuwa askari kufuatana na kawaida ya koo maarufu za wakati huo. Ni baada ya kujeruhiwa sana vitani kwamba aliamua kufuata maisha ya Kiroho badala ya kulenga tena ushindi na heshima ya kidunia[3].
Alipokwenda kuhiji Santiago de Compostela (Hispania) alipitia monasteri kadhaa za Waklunii na kuvutiwa sana na maisha ya namna hiyo.
Aliporudi nyumbani alijitolea mali yake kuanzisha monasteri (1059).
Baadaye alikwenda kupata malezi ya Hugo wa Cluny kwa miaka saba.
Tena akarudi Pontida kuongoza monasteri yake na kuanzisha nyingine kwa wanawake.
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads