Alferi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Alferi, O.S.B. (kwa Kiitalia: Alferio; Salerno, 930 - Cava de' Tirreni, Salerno, 12 Aprili 1050) aliacha mwaka 1002 maisha ya ikulu akawa mmonaki huko Cluny nchini Ufaransa chini ya Odilo.
Baada ya kupata upadirisho huko aliitwa na mtemi wa Salerno akarekebishe monasteri nyingi za huko. Kumbe, baada ya muda alijitenga upwekeni pamoja na wenzake wawili na mwaka 1011 hivi kuanzisha ile maarufu ya Cava akawa abati wake wa kwanza hadi alipofariki dunia akiwa na umri wa miaka 120[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu. Heshima hiyo ilithibitishwa na Papa Leo XIII tarehe 21 Desemba 1893.
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads