Cedd

Askofu wa London; Mtakatifu From Wikipedia, the free encyclopedia

Cedd
Remove ads

Cedd (pia: Cedda, Ceddus; 620 hivi - 26 Oktoba 664) alikuwa mmonaki katika monasteri wa Lindisfarne huko Uingereza, hadi alipotumwa kuinjilisha Waanglia-Saksoni akafanywa na abati Finano wa Lindisfarne askofu wa London.

Thumb
Sanamu za Mt. Albano (kushoto) na Mt. Cedd.

Alijitahidi kufanya uchungaji kwa ukamilifu wa maisha kufuatana na mifano bora ya Mababu wa Kanisa.

Pamoja na mdogo wake Chad wa Mercia[1] anasifiwa kwa kuweka misingi ya Ukristo kati ya Wasaksoni wa Mashariki[2] ambao wakati huo walikuwa na ufukara mkubwa.[3].

Alishiriki Sinodi ya Whitby akipatanisha[4] misimamo ya pande mbili zilizopingana[5].

Pia alianzisha monasteri mbalimbali.

Wote wawili wanaheshimiwa tangu kale kama watakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Oktoba[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads