Daudi wa Wales

From Wikipedia, the free encyclopedia

Daudi wa Wales
Remove ads

David wa Wales (kwa Kiwelisi 'Dewi Sant'; 500 hivi[1] - 589 hivi[2][3]) alikuwa mmonaki wa Welisi, halafu askofu wa Mynyw (sasa inaitwa St Davids kwa heshima yake).

Thumb
Mt. David katika kioo cha rangi, Castell Coch, Cardiff.

Alitunga kanuni ya kimonaki kwa monasteri aliyoianzisha kwa kufuata mfano na desturi za mababu wa mashariki na alipinga vikali Upelaji. Wafuasi wake wengi waliinjilisha Welisi na nchi za kandokando (Ireland, Cornwall na Bretagne).[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na msimamizi wa Wales. Mwaka 1120 Papa Kalisti II alithibitisha heshima hiyo[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Machi[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads