Kiongozi (ndege)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kiongozi (ndege)
Remove ads

Viongozi, vijumbe, walembe au ndege wa asali ni ndege wadogo wa familia Indicatoridae. Kwa kawaida jina “mlembe” hutumika kwa spishi za jenasi Prodotiscus na “kiongozi” kwa spishi nyingine. Ndege hawa wana rangi za kijivu, kahawa na nyeupe, pengine njano pia. Wabobea kwenye kula nta, kwa kawaida nta ya nyuki, lakini walembe na spishi ndogo za viongozi hula nta ya wadudu-gamba. Wanaitwa kiongozi kwa sababu spishi kadhaa (kiongozi mkubwa hasa) huongoza watu na wanyama kama nyegere mpaka masega ya nyuki. Watu au nyegere wakimaliza kutoa asali, kiongozi ala nta inayobaki. Viongozi hula majana, mafunza ya nta, wadudu wengine na buibui pia, na hata matunda mara kwa mara.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...

Viongozi hawatengenezi tago lao lenyewe. Jike hulitaga yai moja katika kila moja la matundu 5 au 6 ya spishi nyingine ya ndege, mara nyingi zile za vigong'ota, zuwakulu na goregore lakini walembe huchagua matago ya mviringo ya vinengenenge, videnenda, magamaga na vibwirosagi. Jike mmoja anaweza kuyataga mayai 20 katika mwaka mmoja. Domo la kinda la kiongozi lina kikulabu kinachotumika kwa kuyatoboa mayai ya mwenyeji na kuwaua makinda yake.

Remove ads

Spishi za Afrika

Remove ads

Spishi za Asia

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads