Waishaak

From Wikipedia, the free encyclopedia

Waishaak
Remove ads

Waishaak (pia Isaaq, Isaac) (kwa Kisomali: Reer Sheekh Isaxaaq, kwa Kiarabu: بني إسحاق bani isḥaq) ni moja ya makabila makubwa kati ya Wasomali.[1]

Ukweli wa haraka Lugha, Dini ...

Wanakalia hasa maeneo ya Somaliland kaskazini mwa Somalia na ya Jimbo la Somali nchini Ethiopia.

Thumb
Picha ya Abdillahi Deria, Sultani Mkuu wa 4 wa Usultani wa Waishaak.
Thumb
Wapiganaji Waishaak wakiwa wamepanda farasi

Kulingana na mapokeo ya jadi ya Wasomali, ukoo wa Waishaak ulianzishwa katika karne ya 13 au 14 wakati alipowasili Ishaaq Bin Ahmed Bin Mohammed Al Hashimi (Sheikh Ishaaq) kutoka Uarabuni aliyezaliwa katika uzao wa Ali ibn Abu Talib.[2] [3] Alikaa katika mji wa pwani wa Maydh kaskazini mashariki mwa Somaliland, ambapo alioa mke kutoka ukoo wa Magaadle. [4]

Kaburi la Sheikh Ishaaq liko Maydh, na ndilo eneo wanapofika mahujaji mara kwa mara. [5] Maulid (siku ya kuzaliwa) ya Sheikh Ishaaq pia huadhimishwa kila Alhamisi kwa kusoma manaaqib yake (mkusanyiko wa matendo matukufu). [4]

Waishaak ndio kabila au ukoo mkubwa wa Wasomali huko Somaliland. Miji mikubwa mitano ya Somaliland - Hargeisa, Burao, Berbera, Erigavo na Gabiley - yote hukaliwa na Waishaak hasa.[6] Vivyo hivyo mikoa mbalimbali ya Somaliland huwa na Waishaak wengi kati ya wakazi yake.[7]

Thumb
Uchoraji wa mwanamke Mishaak uliochapishwa katika Bilder-Atlas mnamo 1870
Remove ads

Historia

Waishaak walishiriki katika vita vya Usultani wa Adal. Baadaye wakati wa karne ya 18 Sultani Guled Abdi alianzisha Usultani wa Waishaak uliodumu kuanzia mwaka 1750 hadi 1884.

Baadaye Waishaak walio wengi waliishi chini ya usimamizi wa Uingereza katika Somalia ya Kiingereza na chini ya utawala wa Ethiopia katika maeneo ya Ogaden.

Wakati wa uhuru mwaka 1960 Somalia ya Kiingereza iliamua kuungana na Somalia ya Kiitalia. Waishaak walishiriki katika harakati ya kuunda Somalia Kubwa iliyolenga kuunganisha pia Wasomali katika Kenya na Ethiopia na nchi ya Somalia.

Wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ya Somalia Waishaak wengi waliuawa na jeshi la dikteta Siad Barre.

Baada ya kuporomoka kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Somalia mnamo 1991, maeneo ya Somaliland yaliyokaliwa na Waishaak hasa yalitangaza uhuru wao kama taifa la pekee. [8]

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads