Liwali
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kwa "wali" kama chakula tazama wali (chakula)

Cheo cha Kiarabu
Asili ni neno la Kiarabu "الوالي" al-wali linalomaanisha mtawala wa mahali au eneo asiyejitegemea bali aliyeteuliwa na serikali kushughulikia mambo ya utawala katika eneo fulani. Mara nyingi katika nchi za utamaduni wa Uislamu Wali alisimamia "wilaya". Kazi yake ililingana na "gavana".
Cheo cha Uswahilini
Katika eneo la Waswahili neno al-wali lilikuwa "liwali"[1] na lilimtaja mkuu wa mahali au wa mji. Masultani wa Zanzibar waliteua maliwali kwa ajili ya miji ya pwani waliokuwa wawakilishi wa sultani mahali walipo.
Mwaka 1886 kulikuwa na maliwali wafuatao wa Zanzibar kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki: Tungi, Mikindani, Lindi, Kilwa Kivinje, Kikunye, Kisiju[2]
Cheo cha kikoloni
Katika mfumo wa utawala wa Kiingereza katika Afrika ya Mashariki liwali ilikuwa cheo cha afisa wa ngazi ya juu zaidi kilichopatikana kwa wazawa katika utawala wa miji.
Cheo hiki kiliendelezwa kwenye pwani ya Kenya baada ya Uingereza kuchukua mamlaka juu ya pwani kutoka Sultani wa Zanzibar; liwali alipaswa kuwa Mwislamu. Alisimamia mahakama ya liwali iliyokuwa ngazi ya juu za mahakama za Kiislamu zilizoamua kesi za mali, ndoa na urithi baina ya Waislamu waliokuwa Waafrika wazalendo au kutoka nchi nyingine, Waarabu au Wahindi[3].
Katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani Wajerumani waliendelea mwanzoni na maliwali waliorithi kutoka kwa Sultani lakini baadaye nafasi yao ilichukuliwa na afisa Mjerumani. Baada ya eneo kutekwa na Uingereza na kuitwa Tanganyika cheo cha liwali kilirudishwa mwaka 1921 kama cheo cha "native administration" ya miji. Kwa mfano mjini Dar es Salaam liwali alikuwa daima Mwislamu kutoka ukoo wa Kiarabu hadi uhuru. Aliwajibika na usimamizi wa mahakama yake alikoshika pia nafasi ya jaji akasimamia pia ukusanyaji wa kodi[4]. Alikuwa na haki ya kuamulia adhabu ya kiboko "hadi viboko sita"[5].
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads