Mbwana Samatta
Mchezaji wa chama cha soka Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mbwana Ally Samatta, (alizaliwa 23 Disemba 1992), ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Tanzania katika klabu ya Feberbahce nchini Uturuki [1]. Mbwana ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars na kabla ya kuhamia klabu ya Feberbahce (Uturuki) alikuwa akucheze timu ya Aston Villa nchini Uingereza[2].
Samatta alianza kucheza soka la kulipwa katika klabu ya African Lyon F.C. mwaka 2008 nchini Tanzania. Alisajiliwa na klabu ya Simba mwaka 2010, ambapo alicheza katika nusu msimu tu kabla ya kujiunga na klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Alicheza kwa miaka mitano ndani ya TP Mazembe na kujijengea nafasi katika kikosi cha kwanza cha klabu hiyo.
Mwaka 2015, alishinda taji la mchezaji bora wa mwaka wa Afrika, na kumaliza msimu akiwa mfungaji bora wa mashindano ya klabu bingwa Afrika (Ligi ya Mabingwa Afrika) na kuisaidia klabu yake kushinda taji hilo.
Samatta alijiunga na klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji mnamo januari 2016, aliisaidia kufuzu michuano ya Ulaya maarufu kama Europa Ligi na kushinda taji la ligi ya Ubelgiji (Belgian Jupiler Ligi mwaka 2019. Alimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa ligi hiyo akashinda tuzo ya mchezaji bora wa ligi ya Ubelgiji (Ebony Shoe award)[3].
Manamo Januari mwaka 2020, Samatta alisajiliwa na klabu ya Aston Villa ya nchini Uingereza na kuwa mchezaji wa kwanza kutoka nchini Tanzania kucheza na kufunga goli ligi kuu ya nchini Uingereza.
Remove ads
Kazi
Samatta alikua mchezaji muhimu wa TP Mazembe waliposhinda taji la klabu bingwa Afrika mwaka 2015 (2015 CAF Champions Ligi), akifunga jumla ya magoli saba na kumaliza akiwa mfungaji bora.[4]
Mnamo Januari 2016, aliposhinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika, aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kutokea Afrika ya Mashariki kutwaa tuzo hiyo. Katika ugawaji wa tuzo hizo uliofanyika jijini Abuja, Nigeria, tarehe 7 Januari 2016, Samatta alikusanya jumla ya alama 127, akimzidi mchezaji mwenzake Robert Kidiaba mlinda lango wa TP Mazembe na timu ya taifa ya DR Congo aliyepata alama 88. Baghdad Bounedjah raia wa Algeria alishika nafasi ya tatu akiwa na alama 63.[5] Katika mchezo dhidi ya Moghreb Tétouan ya Moroko, Samatta alifunga magoli matatu kwa mpigo (hat-trick) yaliyowafanya wasonge hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa Afrika. Magoli hayo yanakumbukwa sana katika historia ya klabu ya TP Mazembe.[6]
Genk
Muda mfupi baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika, alijiunga na klabu ya K.R.C. Genk kwa mkataba wa miaka minne na nusu.[7] Tarehe 23 Agosti 2018 Samatta alifunga goli tatu kwa mpigo(hat-trick) dhidi ya Brøndby IFkwenye mashindano ya Ulaya maarufu kwa jina la Europa Ligi walfanikiwa kupata ushindi wa goli 5–2.[8] Mei 2019 aliishinda tuzo ya mchezaji bora wa ligi ya Ubelgiji (Ebony Shoe).
Aston Villa
Mnamo Januari 20, 2020, Samatta alijiunga na klabu ya Aston Villa inayoshiriki ligi Kuu ya Uingereza kwa mkataba wa miaka minne na nusu.[9] Uhamisho huu ulimfanya Samatta kuwa mchezaji wa kwanza wa kitanzania kucheza ligi kuu ya Uingereza.[10] Ada ya uhamisho inakadiriwa kuwa £8.5 milioni.[11][12] Mchezo wa kwanza alicheza siku nane baada ya kusajiliwa dhidi ya Leceister City kwenye mzunguku wa pili wa mashindano ya Carabao hatua ya nusu fainali, waliibuka na ushindi wa magoli 2 – 1, kwa matoke ohayo, Villa walifika hatua ya fainali.[13]
Samatta alifunga goli lake la kwanza manamo 1 Februari 2020, walipocheza na Bournemouth, mchezo ulimalizika kwa Villa kushinda magoli 2 - 1. Goli hilo lilimfanya Samatta kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kucheza na kufunga kwenye mashindano ya Ligi ya Uingereza.[14]
Fenerbahçe
Samatta alijiunga na Klabu ya Fernabahce ya nchini Uturuki tarehe 25 Septemba 2020, kwa mkopo hadi mwisho wa msimu.[15] Ulipofika mwisho wa mkopo mnamo Julai 2021, Samatta alisaini mkataba wa miaka minne, hii ilikua ni sehemu ya makubaliano ya uhamisho wake.[16]
Tarehe 1 Septemba 2021, Samatta alijiunga na Royal Antwerp ya nchini Ubelgiji kwa mkopo wa msimu mzima.[17]
Ilipofika 16 Agosti 2022, Samatta alirudi tena Genk kwa mkopo, uhamisho huo ulikua na chaguo la Genk kumnunua.[18]
PAOK
Mnamo tarehe 17 Julai 2023, timu ya nchini Ugiriki PAOK ilitangaza kumsajili Samatta kwa mkataba wa miaka miwili, mkataba huo ulikua na nafasi ya kuongeza mwaka mmoja.[19]
Remove ads
Maisha binafsi
Mbwana Samatta ni Mndengereko kutoka Kibiti kwa kabila. Katika maisha ya imani ni Muislamu.[20]
Takwimu za michezo
Klabu
Kimataifa
Magoli Kimataifa
Remove ads
Heshima
TP Mazembe[24]
- Linafoot: 2011, 2012, 2013, 2013–14
- DR Congo Super Cup: 2013, 2014
- Klabu bingwa Afrika: Klabu bingwa Afrka 2015[25][26]
Genk
Binafsi
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads