Mkoa wa Rukwa

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mkoa wa Rukwa
Remove ads

Mkoa wa Rukwa ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Uko kusini mashariki mwa nchi, ukipakana na Mkoa wa Katavi upande wa kaskazini, na mkoa wa Songwe upande wa mashariki, nchi ya Zambia upande wa kusini na huko magharibi Ziwa Tanganyika ndilo mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya kumegwa mwaka 2012 eneo la mkoa lilikuwa takriban km² 70,000. Kwa sasa lina kilomita ya mraba 27,765. Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa wakazi 139,019 [1]. Kusini mwa mkoa liko ziwa Rukwa ambalo ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki na ndilo lililoupatia mkoa jina lake. Makao makuu ya mkoa ni Sumbawanga.

Ukweli wa haraka Nchi, Wilaya ...
Thumb
Mkoa wa Rukwa nchini Tanzania.
Remove ads

Wilaya

Wilaya ziko nne (katika mabano idadi ya wakazi mwaka 2022 [2].):

Wilaya ya Mpanda ilikuwa sehemu ya Rukwa ikawa kiini cha mkoa mpya wa Katavi kuanzia mwaka 2012.

Wakazi

Kabila kubwa zaidi mkoani ndio Wafipa walioko hasa katika wilaya za Sumbawanga na Nkasi. Kati ya makabila mengine kuna Wamambwe-Lungu, Wawanda na Wanyamwanga katika wilaya ya Sumbawanga; kuna pia Wasukuma, Wanyamwezi na Wamasai. Kwa asilimia kubwa wakazi ni waumini wa Kanisa Katoliki.

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

  • Sumbawanga Mjini : mbunge ni Aeshi Hilaly (CCM)
  • Nkansi Kaskazini : mbunge ni Anna Kenani (Chadema)
  • Nkansi Kusini : mbunge ni Deuderit Mipata (CCM)
  • Kwela : mbunge ni Deus Sangu (CCM)
  • Kalambo : mbunge ni Kandege Sinkamba (CCM)

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads