Mkoa wa Katavi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mkoa wa Katavi
Remove ads

Mkoa wa Katavi ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Ulianzishwa rasmi mnamo Machi 2012 kwa kumega sehemu ya kaskazini ya mkoa wa Rukwa. Unapakana pia na mkoa wa Tabora upande wa mashariki na mkoa wa Songwe upande wa kusini. Eneo lake ni la km2 45,843 mashariki mwa ziwa Tanganyika. Katika sensa ya mwaka 2022 idadi ya wakazi ilihesabiwa kuwa 1,152,958 [1]. Makao makuu yako Mpanda.

Ukweli wa haraka Nchi, Kanda ...

Una postikodi namba 50000

Remove ads

Wilaya

Wilaya za mkoa huo ni tano tu: Mlele, Nsimbo, Mpanda mjini, Tanganyika (awali Mpanda vijijini) na Mpimbwe.

Utamaduni

Kabila kubwa ni lile la Wafipa; pia kuna Wabende, Wapimbwe na Wakonongo na dini yao kwa kiasi kikubwa sana ni Ukristo wa madhehebu ya Kanisa Katoliki.

Wapimbwe wanapatikana katika maeneo ya wilaya ya Mpimbwe katika vijiji vya Mamba, Mpimbwe na Majimoto. Katika kijiji cha Mamba kuna kivutio kizuri: bwawa kubwa la asili la maji ya moto ambayo hayapoi muda wote, ni ya moto iwe mchana au usiku.

Pia kuna sehemu za mkoa huu ni wa kihistoria katika baadhi ya maeneo. Mfano mtaa wa Madukani ambao walikua wakiishi Wahindi na Waarabu wa Oman kama Mzee Yusuf Al Salmi.

Remove ads

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

  • Katavi : mbunge ni Issack Kamwele (CCM)
  • Kavuu : mbunge ni Dk. Pudenciana Kikwembe (CCM)
  • Mpanda Mjini : mbunge ni Sebastian Kapufi (CCM)
  • Mpanda Vijijini : mbunge ni Moshi Selemani Kakoso (CCM)
  • Nsimbo : mbunge ni Richard Mbogo (CCM)

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads