Modesti wa Yerusalemu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Modesti wa Yerusalemu
Remove ads

Modesti wa Yerusalemu (Sivas, Kapadokia, leo nchini Uturuki, karne ya 617 Desemba 630[1]) alikuwa askofu wa mji huo nchini Israeli.

Thumb
Masalia ya Mt. Modesti wa Yerusalemu panapotunzwa.

Kabla ya hapo aliuzwa kama mtumwa kwenda Misri. Huko alimuongoa bwana wake ambaye alimuacha huru. Hapo alijiunga na umonaki kwenye mlima Sinai. Baadaye akafanywa abati wa monasteri huko Palestina.

Mwaka 614 Kosroe II wa Persia aliteketeza Yerusalemu akiua Wakristo 66,509. Modesti alichaguliwa kushika nafasi ya askofu Zakaria aliyetekwa, na huyo alipofariki Modesti akawa askofu. Alijitahidi sana kujenga upya monasteri kadhaa hata zikajaa wamonaki na makanisa yaliyoteketezwa kwa moto [2][3].

Tangu kale ametambuliwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 17 Desemba[4] na nyinginezo.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads