Papa Gelasio I
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Papa Gelasio I alikuwa Papa kuanzia tarehe 1 Machi 492 hadi kifo chake tarehe 21 Novemba 496[1]. Alikuwa Papa wa tatu mwenye asili ya Afrika kaskazini.[2][3][4]

Alimfuata Papa Felix III akafuatwa na Papa Anastasio II.
Maarufu kwa ujuzi na uadilifu, alidai utiifu kwake kutoka kwa Wakristo wa Magharibi na Mashariki vilevile na kutetea kwa nguvu imani sahihi hata kuchangia mabishano, ingawa alikuwa na mahusiano mazuri na watawala Waostrogoti waliokuwa Waario[5].
Akisukumwa na upendo wake mkubwa na mahitaji ya maskini, ili kuwasaidia yeye mwenyewe alifariki fukara sana [6].
Remove ads
Maandishi
Mwandishi mahiri[7], kati ya Mapapa wa karne za kwanza, ndiye aliyeandika zaidi.
Mwaka 494, aliandika barua Duo sunt kwa kaisari Anastasius I kuhusu mahusiano ya Kanisa na Dola; barua hiyo aliathiri siasa kwa karibu miaka elfu.[8] Ili kuzuia mamlaka ya kaisari isidhuru umoja wa Kanisa, alichambua kwa dhati sifa za mamlaka hiyo ya kidunia na za ile ya kiroho, akisisitiza haja ya kila upande kuwa huru.
Pia zimetufikia barua zake nyingine zaidi ya 100[9]. Maandishi mengine yalitajwa kuwa ya kwake ingawa si kweli; lengo lilikuwa kuyatia maanani zaidi.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sikukuu yake ni tarehe 21 Novemba[10].
Remove ads
Tazama pia
Maandishi yake
- Opera Omnia katika Patrologia Latina ya Migne pamoja na faharasa
- Duo sunt: introduction and text in English
- Decretum Gelasianum: De Libris Recipiendis et Non Recipiendis Ilihifadhiwa 20 Agosti 2008 kwenye Wayback Machine.
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads