Papa Linus
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Papa Linus alikuwa Papa kuanzia takriban 68 hadi kifo chake takriban 79[1]. Alitokea mkoa wa Toscana, Italia[2].

Alimfuata Papa wa kwanza[3], Mtume Petro[4][5][6][7][8][9], akafuatwa na Papa Anacletus.
Ndiye aliyetajwa na Mtume Paulo katika Waraka wa pili kwa Timotheo, 4:21[10] kwamba alikuwa naye mwishoni mwa maisha yake[11].
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu na kutajwa katika Kanuni ya Kirumi.
Sikukuu yake ni tarehe 23 Septemba[12].
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads