Papa Celestino I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Celestino I
Remove ads

Papa Celestino I alikuwa Papa kuanzia tarehe 10 Septemba 422 hadi kifo chake tarehe 24 Julai 432[1]. Alitokea Campania, Italia na baba yake aliitwa Priscus.

Thumb
Mtakatifu Selestino I.

Alimfuata Papa Boniface I akafuatwa na Papa Sixtus III.

Akiwa na juhudi za kulinda na kupanua Kanisa, alianzisha uaskofu katika visiwa vya Britania akaunga mkono Mtaguso wa Efeso katika kumuita Bikira Maria "Mama wa Mungu" dhidi ya mafundisho ya Nestori[2].

Alipambana pia na uzushi wa Upelaji [3] na kupigania nidhamu[4][5] pamoja na kudhibiti farakano la Novatianus[6].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 27 Julai[7] lakini pia 6 Aprili au 8 Aprili.

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads