Papa Yohane I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Yohane I
Remove ads

Papa Yohane I alikuwa Papa kuanzia tarehe 13 Agosti 523 hadi kifo chake tarehe 18 Mei 526[1]. Alitokea Toscana, Italia[2].

Thumb
Mt. Yohane I.

Alimfuata Papa Hormisdas akafuatwa na Papa Felisi IV.

Alitumwa na mfalme Theodoriko Mkuu kwa Kaisari Yustino I wa Konstantinopoli[3][4] ili Waario wasiendelee kudhulumiwa. Alikuwa Papa wa kwanza kuadhimisha sadaka ya Pasaka katika mji huo. Ingawa alifaulu walau kiasi katika lengo la mfalme, aliporudi Italia alifungwa naye hadi akafa kwa magumu yaliyompata gerezani [5].

Tangu kale ameheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 18 Mei[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads