Papa Zakaria

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Zakaria
Remove ads

Papa Zakaria alikuwa Papa kuanzia tarehe 3 Desemba 741 hadi kifo chake tarehe 15 Machi 752[1]. Alitokea Ugiriki[2] au Santa Severina, Calabria, Italia, labda akiwa na asili ya Balkani.

Thumb
Mt. Zakaria Papa.

Jina la baba yake lilikuwa Polichronios.

Alimfuata Papa Gregori III akafuatwa na Papa Stefano II[3].

Anasifiwa sana na wanahistoria mbalimbali kwa jinsi alivyokabili vizuri mazingira magumu na ya hatari[4], akiongoza familia ya Mungu kwa umakinifu na busara ya hali ya juu [5].

Alifaulu kupatana na Walombardi walioteka sehemu kubwa ya Italia[6] au kupunguza ukali wao, aliwaelekeza Wafaranki namna ya kutawala kwa haki na kumhimiza Pipino Mfupi kujifanya rasmi mfalme wao[7], alifanya makabila ya Kijerumani yawe na makanisa zaidi, aliunga mkono umisionari wa Bonifas huko Ujerumani[8], alidumisha umoja na Kanisa la Mashariki, alipinga sera ya kaisari Konstantino V dhidi ya picha takatifu[7], alidhibiti mwelekeo wa kutunga majina kwa malaika[9] na alikataza biashara ya watumwa mjini Roma akiwakomboa waliokwisha kuletwa[6][10][11].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Machi[12].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads