Perpetui wa Tours

From Wikipedia, the free encyclopedia

Perpetui wa Tours
Remove ads

Perpetui wa Tours (alifariki Tours, leo nchini Ufaransa, 30 Desemba 490 BK) alikuwa askofu wa 6 wa mji huo kwa miaka 30 baada ya ndugu yake Eustoki wa Tours na kabla ya ndugu yake mwingine, Volusiano wa Tours.

Thumb
Mt. Perpetui katika mavazi ya ibada ya kiaskofu.

Alijenga basilika la Mt. Martino na makanisa mengine mengi kwa heshima ya watakatifu pamoja na kurudisha jimboni mwake desturi ya kufunga chakula na kukesha [1].

Gregori wa Tours aliandika juu yake[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Desemba[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads