Stefano Harding

From Wikipedia, the free encyclopedia

Stefano Harding
Remove ads

Stefano Harding (Sherborne, Dorset, Uingereza, 1060 hivi - Citeaux, Ufaransa, 28 Machi 1134) alikuwa mmonaki[1], padri, mwanzilishi mmojawapo[2] na abati[3] wa urekebisho wa Citeaux wa shirika la Benedikto wa Nursia.

Thumb
Mchoro wa ukutani wa Mt. Stefano Harding.

Alifika Cîteaux kutoka Molesme pamoja na wamonaki wengine, akaongoza monasteri hiyo na kuanzisha huko tabaka la mabradha.

Katika uongozi wake wa miaka 25 aliongeza monasteri 12 alizoziunganisha chini ya Mwandiko wa Upendo, ili kusiwe na ugomvi wowote kati ya wamonaki bali wote waishi kwa kufuata amri ya upendo, kanuni moja na desturi za kufanana. Ndiye aliyempokea utawani Bernardo wa Clairvaux na wenzake 30[4][5].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 28 Machi[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads