Thomas Garnet

From Wikipedia, the free encyclopedia

Thomas Garnet
Remove ads

Thomas Garnet, S.J. (Southwark, 1575 hivi – Tyburn, 23 Juni 1608) alikuwa padri Mjesuiti kutoka Uingereza aliyeuawa kwa kuwa Mkatoliki chini ya mfalme James I[1].

Thumb
Mt. Thomas Garnet alivyochorwa.

Baada ya kusoma huko Ufaransa na Hispania, alipadrishwa akarudi Uingereza (1599) alipofanya utume kwa kificho miaka 6 hadi alipokamatwa kwa mara ya pili. Miezi baadaye alifukuzwa nchini kwa tishio la kuuawa akirudi tena.

Alipomaliza unovisi katika shirika huko Louvain, alitumwa Uingereza alipokamatwa wiki 6 tu baadaye akauawa kwa kukataa kiapo cha kumtii mfalme badala ya Papa[2].

Alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenyeheri tarehe 15 Desemba 1929, na Papa Paulo VI kuwa mtakatifu mfiadini tarehe 25 Oktoba 1970.

Sikukuu yake ni tarehe 23 Juni [3]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads