Yosefu Cafasso

From Wikipedia, the free encyclopedia

Yosefu Cafasso
Remove ads

Yosefu Cafasso (kwa Kiitalia Giuseppe Cafasso; 15 Januari 1811 - 23 Juni 1860) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mwanaharakati kutoka Piemonte, Italia.

Thumb
Mt. Yosefu Cafasso.

Pamoja na watakatifu Yosefu Benedikto Cottolengo, Yohane Bosco, Maria Dominika Mazzarello na Leonardo Murialdo aliwajibika kukabili matatizo ya jamii katika mji mkuu wa ufalme wa Sardinia, Torino. Hasa alishughulikia wafungwa na waliohukumiwa kufa ili kuwapatanisha na Mungu.

Pia aliwajibika kwa malezi ya kielimu na ya kiroho ya wenye wito wa upadri[1]

Cafasso alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenye heri mwaka 1925, halafu na Papa Pius XII kuwa mtakatifu mwaka 1947.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads