From Wikipedia, the free encyclopedia
Rosa wa Viterbo (Viterbo, leo mkoani Lazio, Italia, 1233 hivi – 6 Machi 1251[1] ) alikuwa msichana maarufu kwa imani yake katika Ukristo aliyejiunga mapema sana na Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko.
Baada ya kuishi kama mkaapweke kuanzia umri wa miaka 7, alianza kuhubiri toba na upatanisho hata alipofukuzwa mjini (1250).
Mwaka huohuo, baada ya Papa kuteka tena Viterbo, alirudishwa kutokana na karama zake za uponyaji na unabii, lakini akafariki mapema kutokana na afya yake mbovu toka zamani.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mwenye heri bikira.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Machi[2] au 4 Septemba, siku ambapo maiti wake asiyeoza ardhini alihamishiwa kanisani (1258). Mpaka leo moyo wake ni mzima.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.