Galdino wa Sala

From Wikipedia, the free encyclopedia

Galdino wa Sala
Remove ads

Galdino wa Sala (1096 hivi [1]18 Aprili 1176) alikuwa kardinali tena askofu mkuu wa Milano, Italia Kaskazini, miaka 1166-1176.[2]

Thumb
Masalia yake katika kanisa kuu la Milano.

Kwa nguvu zote aliunga mkono juhudi za Papa Alexander III, za Milano na za miji mingine ya Lombardia, dhidi ya Antipapa Victor IV (11591164) aliyetegemezwa na kaisari Frederick I Barbarossa.

Alihamasisha matengenezo ya mji ulioharibiwa na vita vya kupigania mamlaka.

Anakumbukwa pia kwa ukarimu wake kwa mafukara na kwa waliofungwa kutokana na madeni.

Alifariki baada ya kutoa hotuba dhidi ya wazushi.

Papa Alexander III mwenyewe alimtangaza mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 18 Aprili[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads