Henry VIII wa Uingereza

From Wikipedia, the free encyclopedia

Henry VIII wa Uingereza
Remove ads

Henry VIII (28 Juni 1491 28 Januari 1547) alikuwa mfalme wa Uingereza kuanzia tarehe 21 Aprili 1509 hadi kifo chake. Ni wa pili kutoka nasaba ya Tudor, akimfuata baba yake, Henry VII.

Thumb
Mfalme Henri VIII alivyochorwa na Hans Holbein the Younger, Walker Art Gallery, Liverpool, Uingereza.

Maisha na matukio

Wake sita wa Henry VIII
(kufuatana na mwaka wa ndoa)
Thumb
Katarina wa Aragon
(1509–1533)
Thumb
Anne Boleyn
(1533–1536)
Thumb
Jane Seymour
(1536–1537)
Thumb
Anne of Cleves
(1540)
Thumb
Catherine Howard
(1540–1542)
Thumb
Catherine Parr
(1543–1547)

Henry anajulikana hasa kwa kuoa wanawake sita, mmoja baada ya mwingine, na hasa kwa juhudi zake za kubatilisha ndoa yake ya kwanza na Katerina wa Aragona zilizomfanya hatimaye atenganishe Kanisa la Uingereza na Papa, akijifanya mkuu wa Kanisa. Pamoja na kutengwa na Kanisa Katoliki kwa sababu hiyo, aliendelea kusadiki mafundisho yake.[1]

Katika masuala ya ndani, Henry alijulikana kwa kubadilisha sana katiba ya nchi, akizidisha mamlaka yake mwenyewe. Waliopinga walishutumiwa kama wasaliti na mara nyingi kuhukumiwa adhabu ya kifo, akiwemo waziri mkuu Thomas More.

Matumizi yake yalikuwa makubwa mno, kwa ajili ya fahari na vita, hivi kwamba pesa nyingi alizofaulu kujipatia kwa kuteka mali ya monasteri na kuzuia kodi iliyokuwa inalipwa awali kwa Papa, hazikumtosha kamwe.

Aliunganisha Uingereza na Wales akawa pia mfalme wa kwanza wa Uingereza kushika nafasi ya mfalme wa Ireland.

Mwanzoni wengi walipendezwa naye[2], lakini baadaye alizidi kunenepa, afya yake ilitetereka, na hata nafsi yake ilivurugika na kumfanya mzinzi, mkatili, mwoga.[3]

Baada yake alitawala mwanae Edward VI.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads