Kiukraini

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kiukraini
Remove ads

Kiukraini (kwa Kiukraini: українська (мова), ukrajins'ka mova) ni lugha ya Kislavoni cha Mashariki, mojawapo katika familia ya Lugha za Kihindi-Kiulaya.

Kiukraini kinavyozungumzwa.
Maelezo zaidi Lugha rasmi:, Uainishaji wa kiisimu: ...
Thumb
Uenezi wa Kiukraini duniani.

Kiukraini ni lugha ya pili inayozungumzwa zaidi katika orodha ya lugha za Kislavoni. Kuna waongeaji milioni 37 wanaoongea lugha hiyo nchini Ukraini, ambapo ni lugha rasmi. Kwa wengi wa wenyeji wake lugha hiyo ni lugha mama. Kwa hesabu ya dunia nzima, kuna waongeaji wapatao milioni 47 wanaoongea lugha hiyo.

Lugha ya Kiukraini huandikwa kwa herufi za Kisirili.

Remove ads

Alfabeti

Alfabeti ya Kiukraini kwa tafsiri ya maelezo kuelekea Kijerumani:

Maelezo zaidi Groß (HTML-Entity), Klein (HTML-Entity) ...
Remove ads

Kupiga marufuku lugha ya Kiukraini

Thumb
Agizo la Piotr Valuev la 1863 lililokataza kuzungumza Kiukreni

Uharibifu wa Cossacks mwaka 1775 ulisababisha utumwa wa Waukraini na sera ya Urusishaji (kwa Kirusi: Русификация) - kupiga marufuku rasmi na uharibifu wa lugha na utamaduni wa Kiukraini na wakoloni wa Kirusi. Mfano wa kushangaza zaidi wa sera kama hiyo ni Amri ya Ems (kwa Kirusi: Эмский указ) na amri ya Piotr Valuev (kwa Kirusi: Валуевский циркуляр) Waziri wa Mambo ya Ndani ya Dola la Urusi, hati hii kutoka mwaka 1863 ilisema kwamba lugha ya Kiukraini "haikuwepo, haipo na haiwezi kuwepo, na mtu yeyote ambaye hakubaliani na taarifa hii ni adui wa Urusi." [1][2]. Pia wakati wa Umoja wa Kisovyeti matumizi yake yalikuwa machache sana [3].

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads