Mkoa wa Pwani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mkoa wa Pwani ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepakana upande wa Kaskazini na mkoa wa Tanga, upande wa mashariki na Dar-es-Salaam na Bahari Hindi, upande wa kusini na mkoa wa Lindi na upande wa magharibi na mkoa wa Morogoro. Mkoa huo una eneo la km² 32,407, na idadi ya wakazi wapatao 2,024,947 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1] kutoka 1,098,668 (2012). Mkoa huo ni maarufu kwa shughuli za utalii hususani katika mji wa Bagamoyo, kisiwa cha Mafia na Hifadhi ya Taifa ya Saadani. Makao makuu ya mkoa yako Kibaha.

Kwa mkoa wa zamani wa Kenya, tazama Mkoa wa Pwani (Kenya).

Remove ads
Wilaya na wakazi
Mkoa wa Pwani una wilaya nane (katika mabano idadi ya wakazi wakati wa sensa ya mwaka 2022 [2]):
- Bagamoyo (205,478)
- Chalinze (316,759)
- Kibaha Mjini (265,360)
- Kibaha Vijijini (123,367)
- Kisarawe (159,226)
- Mkuranga (533,033)
- Mafia (66,180)
- Rufiji (159,906)
- Kibiti (195,638).
Mkoa huo wenyeji wake ni watu wa makabila ya Wakwere, Wazaramo, Wandengereko, Wadoe, Wazigua na Wanyagatwa.
Remove ads
Majimbo ya bunge
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huo ulikuwa na majimbo ya uchaguzi tisa yafuatayo [3]:
- Chalinze : mbunge ni Ridhwan Kikwete (CCM)
- Bagamoyo : mbunge ni Shukuru Kawambwa (CCM)
- Kibaha Mjini : mbunge ni Sylvester Francis Koka (CCM
- Kibaha Vijijini : mbunge ni Hamoud Abuu Jumaa (CCM)
- Kisarawe : mbunge ni Selemani Said Jafo (CCM)
- Mafia : mbunge ni Mbaraka Kitwana Dau (CCM)
- Mkuranga : mbunge ni Abdallah Hamis Ulega (CCM)
- Kibiti : mbunge ni Ally Seif Ungando (CCM)
- Rufiji : mbunge ni Mohamed Omary Mchengerwa (CCM)
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads