Nikola Tavelic

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nikola Tavelic
Remove ads

Nikola Tavelić (Šibenik, Korasya, 1340 hivi - Yerusalemu, leo kati ya Israeli na Palestina, 14 Novemba 1391) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo, padri na mmisionari katika Nchi takatifu ya Yesu.

Thumb
Kioo cha rangi chenye picha ya Mt. Nikola Tavelic huko Rijeka.
Thumb
Ua wa monasteri ya zamani ya Mlima Sion huko Yerusalemu, alipoishi Mt. Nikola.

Pamoja na wenzake Deodato wa Ruticinium, Stefano wa Cuneo na Petro wa Narbone, alichomwa moto kwa kuwa walihubiri hadharani kwa ushujaa dini ya Kikristo mbele ya Waislamu, wakimkiri kwa uimara Kristo Mwana wa Mungu [1].

Pamoja nao alitangazwa na Papa Leo XIII kuwa mwenye heri mwaka 1889, halafu na Papa Paulo VI kuwa mtakatifu mfiadini tarehe 21 Juni 1970. Ni wa kwanza kutoka Kroatia.

Sikukuu yao ni tarehe waliyouawa na Waislamu waliowahubiria Injili[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads