Papa Eleutero

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Eleutero
Remove ads

Papa Eleutero (kwa Kigiriki Ελευθέριος) alikuwa Papa kuanzia takriban 171/177 hadi kifo chake takriban 185/193[1]. Alitokea Nikopoli, Ugiriki.

Thumb
Papa Eleutero.

Alimfuata Papa Soter akafuatwa na Papa Viktor I.

Egesipo aliandika kwamba alikuwa shemasi wa Roma chini ya Papa Aniseti na Papa Soter.

Chini yake uzushi ulienea [2] na Eleutero aliandika kitabu kuupinga [3]

Wafiadini wa Lyon, wakiwa gerezani, walimuandikia barua nzuri sana kuhusu kudumisha amani ya Kanisa[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Mei[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads