Papa Sergio I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Sergio I
Remove ads

Papa Sergio I alikuwa Papa kuanzia tarehe 15 Desemba 687 hadi kifo chake tarehe 7 Septemba 701[1]. Alitokea Syria[2] au alizaliwa Palermo (Italia) katika familia kutoka Syria[3].

Thumb
Mt. Sergio I.

Alimfuata Papa Konon[4][5][5][6][7] akafuatwa na Papa Yohane VI.

Alipigania kwa nguvu zote uinjilishaji wa Wasaksoni na Wafrisia akamfanya mmisionari Wilibrodi kuwa askofu wao.

Pia alimaliza farakano la Akwileia (698)[5] na migogoro mingine, lakini alikuwa tayari kuuawa kuliko kukubali uzushi[8].

Hivyo alikataa kabisa[9][10] kuthibitisha kanuni zilizotungwa na maaskofu wa Mashariki[11] katika Mtaguso wa tano-sita zikilenga kufanya desturi za Konstantinopoli zifuatwe na Wakatoliki wote[12][13]. Kwa sababu hiyo kaisari Justiniani II aliagiza akamatwe na kuletwa Konstantinopoli, lakini watu walizuia utekelezaji wa amri hiyo[5][14].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, hasa tarehe 8 Septemba [15].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads