Nyanda za chini za Turan

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nyanda za chini za Turan
Remove ads

Nyanda za chini za Turan (kwa Kiingereza: Turan Depression, Turanian Basin) ni eneo tambarare la km² milioni 1.9 lililopo duni kuliko mazingira yake katika Asia ya Kati. Linaenea katika Turkmenistan kupitia Uzbekistan hadi Kazakhstan, tariban baina ya Bahari ya Kaspi na Ziwa Aral. Asilimia 80 ni jangwa la mchanga au la chumvi.

Thumb
Ramani ya bahari ya Kaspi na Ziwa Aral, kivuli cha manjano kinaonyesha beseni la Kaspi.

Mvua ni haba na uoto ni mimea midogo, nyasi na vichaka vidogo vinavyofaa kama lishe ya kondoo na ngamia lakini penye oasisi watu wamekuwa wakilima pia tangu kale.[1].

Kwa wastani, eneo hilo hupata chini ya mm 381 za mvua kwa mwaka. Jangwa la Kara Kum linapatikana kusini mwa Nyanda za chini za Turan.

Miji mitatu mikubwa zaidi ni: Daşoguz huko Turkmenistan, Nukus katika Uzbekistan, na Urganch, pia katika Uzbekistan.

Sehemu za chini zaidi ziko Turkmenistan zikiwa mita 81 chini ya usawa wa bahari .

Mito ya Amu Darya na Syr Darya hutiririsha maji kutoka milima ya Pamir na Tien Shan hadi Ziwa Aral kuvukia majangwa haya.

Kimataifa eneo lina umuhimu wa kiuchumi kutokana na akiba za gesi asilia na mafuta ya petroli katika mazingira ya Bahari Kaspi[2].

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads