WhatsApp

emmanuel ngwisia lifwenyi amezaliwa mwaka wa 28/12/ 1986 katika mji wa nakuru From Wikipedia, the free encyclopedia

WhatsApp
Remove ads

WhatsApp ni mtandao wa kijamii unaotumika kutuma ujumbe wa maneno, sauti, picha au video unaomilikiwa na kampuni ya Facebook.[3] Teknolojia hii ilianzishwa na kampuni ya WhatsApp Inc. ya Mountain View, California ambayo baadaye ilinunuliwa na Facebook mnamo Februari 2014 kwa gharama ya dola za Kimarekani bilioni 19.3.[4][5]

Ukweli wa haraka Wandishi wa sasa, Tarehe ya kwanza ...
Ukweli wa haraka Tarehe ya kwanza, Mwanzilishi ...
Thumb
Mtu akituma ujumbe kwa kutumia WhatsApp.

WhatsApp inatumiwa hasa kwenye simu za mkononi ingawa inaweza pia kutumika kwenye kompyuta.[6]

Mwanzoni watumiaji walikuwa wanaweza kuwasiliana na watumiaji wengine mmoja mmoja au katika kundi lakini toka Septemba 2017 WhatsApp ilitangaza kuanzisha utaratibu wa makampuni kuwasiliana na wateja wao.[7]

Hadi Februari 2018, WhatsApp ilikuwa na watumiaji zaidi ya bilioni moja na nusu. [8]

Teknolojia hii imeimarika katika nchi kadhaa kama vile Brazili, India, nchi kadhaa za Ulaya kama vile Uingereza na Ufaransa.[9]

Huduma ya kutumia WhatsApp kupiga simu ilianza kutumika Februari 2015. [10][11]. Tarehe 14 Novemba 2016 WhatsApp ilianzisha huduma ya kupiga simu kwa video kwa simu zinazotumia android, simu za iPhone na Windows.[12]

Tarehe 18 Januari 2016, mwanzilishi wa WhatsApp Jan Koum alitangaza kuwa kampuni hii haitatoza dola 1 ya Marekani kwa matumizi ya WhatsApp mwaka mmoja ili kuondoa tatizo lililokuwa linawasumbua watumiaji wasio na njia ya kulipa. Alitangaza pia kuwa kampuni hii haitaweka matangazo ya kampuni nyingine na badala yake itaimarisha huduma nyingine kama vile mawasiliano ya watumiaji na makampuni. Gharama ya WhatsApp huwa ni gharama watumiaji wanayolipa ili kutumia intaneti kwenye makampuni ya simu. Gharama hii hutofautiana kati ya nchi na nchi na pia kati ya kampuni za simu.

Remove ads

Historia

WhatsApp ilianzishwa na Brian Acton na Jan Koum mnamo mwaka 2009. Wote wawili walikuwa wafanyakazi wa zamani wa Yahoo! Kabla ya kuanzisha WhatsApp, waliona umuhimu wa kuwa na njia rahisi na ya haraka ya mawasiliano kwenye simu za mkononi.

WhatsApp ilitoka kama suluhisho la kutoza ada ya kila mwaka kwa watumiaji wake, badala ya kutegemea matangazo au mauzo ya data. Modeli hii ya biashara ilisaidia kudumisha faragha ya watumiaji kwa kiwango kikubwa. Huduma ilipata umaarufu haraka kutokana na urahisi wake wa matumizi, ujumuishaji wa nambari za simu kama kitambulisho, na uwezo wa kutoa mawasiliano ya haraka kwa njia ya ujumbe wa maandishi.

Mnamo mwaka 2014, WhatsApp ilinunuliwa na kampuni ya Facebook kwa dola bilioni 19. Hata baada ya ununuzi huo, WhatsApp ilijitahidi kudumisha sifa yake ya faragha na kutofautisha kati ya data ya WhatsApp na akaunti za Facebook. Hata hivyo, mabadiliko kadhaa yamefanywa kwa muda kuhusu sera za faragha, na mjadala kuhusu hili umeibuka mara kwa mara.

WhatsApp imeendelea kuwa mojawapo ya programu maarufu duniani kwa mawasiliano ya simu ya mkononi na inaendelea kuboreshwa na kupanuliwa na Facebook.

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads