Eusebius wa Vercelli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Eusebius wa Vercelli (kisiwa cha Sardinia, 2 Machi 283 hivi – Vercelli, Piemonte, 1 Agosti 371) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki katika karne ya 4, wa kwanza katika mji huo wa Italia Kaskazini.


Alikusanya mapadri wa jimbo lake kuishi kimonaki na kuimarisha Ukristo katika eneo lote karibu na milima ya Alpi.
Pamoja na Atanasi wa Aleksandria alitetea imani katika umungu wa Yesu dhidi ya Waario na kwa ajili hiyo aliteswa na kupelekwa na kaisari Konstans uhamishoni Palestina, Kapadokia na hadi jangwa la Misri.
Miaka 8 baadaye aliweza kurudi jimboni mwake akaendelea na umisionari wake pamoja na kuimarisha waumini katika imani sahihi [1].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.
Remove ads
Tazama pia
Maandishi yake
- Toleo jipya la maandishi yake linapatikana katika gombo la 9 la Corpus Christianorum - Series Latina.
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Marejeo ya lugha nyingine
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads