Eusebius wa Vercelli

From Wikipedia, the free encyclopedia

Eusebius wa Vercelli
Remove ads

Eusebius wa Vercelli (kisiwa cha Sardinia, 2 Machi 283 hivi – Vercelli, Piemonte, 1 Agosti 371) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki katika karne ya 4, wa kwanza katika mji huo wa Italia Kaskazini.

Thumb
Bikira Maria katika utukufu pamoja na Malaika Gabrieli, na watakatifu Eusebius wa Vercelli (ameketi), Sebastiano na Roko katika mchoro wa Sebastiano Ricci.
Thumb
Sehemu ya Codex Vercellensis, inayodhaniwa kuwa iliandikwa na Eusebius mwaka 370.

Alikusanya mapadri wa jimbo lake kuishi kimonaki na kuimarisha Ukristo katika eneo lote karibu na milima ya Alpi.

Pamoja na Atanasi wa Aleksandria alitetea imani katika umungu wa Yesu dhidi ya Waario na kwa ajili hiyo aliteswa na kupelekwa na kaisari Konstans uhamishoni Palestina, Kapadokia na hadi jangwa la Misri.

Miaka 8 baadaye aliweza kurudi jimboni mwake akaendelea na umisionari wake pamoja na kuimarisha waumini katika imani sahihi [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Agosti[2].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

  • Toleo jipya la maandishi yake linapatikana katika gombo la 9 la Corpus Christianorum - Series Latina.

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads