Fransisko Saveri

From Wikipedia, the free encyclopedia

Fransisko Saveri
Remove ads

Fransisko Saveri (jina asili: Francisco de Jasso y Azpilicueta; Javier, Navarra, leo nchini Hispania, 7 Aprili 1506 - kisiwa cha Shangchuan, China, 3 Desemba 1552) alikuwa padri wa Shirika la Yesu, ambalo alichangia kulianzisha pamoja na Ignas wa Loyola.

Thumb
Fransisko Saveri akimuongoa Paravas huko Goa, India, katika picha ya karne ya 19.
Thumb
Safari zake.
Thumb
Ngome ya familia ya Xavier.
Thumb
"Njozi ya Mt. Fransisko SaverI", ilivyochorwa na Giovanni Battista Gaulli.
Thumb
Kioo katika kanisa la Hong Kong kikimchora akimbatiza Mchina.
Thumb
Kanisa la Saint-Pierre de Montmartre, Paris, alipoweka nadhiri zake.
Thumb
Kaburi lake katika Basilika la Yesu Mwema huko Goa.

Baadaye, akisukumwa na hamu yenye ari ya kueneza Injili, alimtangaza Kristo kwa bidii katika nchi nyingi za Ulaya, Afrika na Asia hata akawa kati ya wamisionari maarufu zaidi ya historia ya Kanisa.

Baada ya kuwahubiria makabila mengi ya India, visiwa vya Maluku na vinginevyo, huko Japani aliongoa watu wengi kwenye imani ya Ukristo akafa hatimaye karibu na China bara, ameishiwa nguvu na maradhi na kazi nyingi[1].

Alitangazwa na Papa Paulo V kuwa mwenye heri tarehe 25 Oktoba 1619, halafu Papa Gregori XV akamtangaza mtakatifu tarehe 12 Machi 1622.

Anaheshimiwa na Waanglikana na Walutheri pia.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2]

Remove ads

Sala yake

Ee Mungu wa mataifa yote ya dunia, uukumbuke umati wa Wapagani ambao, ingawa waliumbwa kwa sura yako, hawajakufahamu wewe wala kifo cha Mwanao Yesu Kristo, mwokozi wao.

Fanya kwamba, kwa sala na kazi za Kanisa lako takatifu, wakombolewe kutoka ushirikina wote na utovu wa imani wakaletwe kwenye ibada zako.

Kwa njia ya yule uliyemtuma awe ufufuo na uzima wa watu wote, huyo Mwanao Yesu Kristo, Bwana wetu.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads