Maria kutolewa hekaluni

From Wikipedia, the free encyclopedia

Maria kutolewa hekaluni
Remove ads

Bikira Maria Kutolewa Hekaluni ni kumbukumbu ya liturujia inayoadhimishwa na Wakatoliki na Waorthodoksi tarehe 21 Novemba[1][2].

Thumb
Mchoro wa ukutani huko Skopje, Macedonia.
Thumb
Mchoro wa Titian (1534-1538, Gallerie dell'Accademia, Venice).

Msingi

Adhimisho linatokana na habari ambayo haipatikani katika Agano Jipya, ila katika Injili ya Yakobo. Humo inasimuliwa kwamba wazazi wa Bikira Maria, Yohakimu na Ana, ambao hawakuwa na watoto, walipata ujumbe kutoka mbinguni kwamba watapata mtoto.

Kama shukrani ya kupata mtoto wa kike, akiwa bado mdogo walimleta katika Hekalu la Yerusalemu ili kumweka wakfu kwa Mungu[3].

Huko alibaki hadi alipotolewa kwa Yosefu.[3][4]

Kwa namna nyingine, inaaminika kwamba mwenyewe alijitoa mapema kwa Mwenyezi Mungu, yeye aliyejaa neema tangu kutungwa mimba kwa kukingiwa dhambi ya asili na atakayejaliwa kuwa Mama wa Mungu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu [5].

Remove ads

Asili

Sikukuu ilianzishwa kuhusiana na kutabaruku Basilika jipya la Mtakatifu Maria, lililojengwa mwaka 543 na kaisari Justinian I karibu na mabaki ya Hekalu la Yerusalemu.[4]

Kutoka Ukristo wa mashariki sikukuu ilienea katika monasteri za Italia Kusini katika karne ya 9, ikaingia katika liturujia ya Papa wa Avignon mwaka 1372 kwa agizo la Papa Gregori XI.[6][7]

Picha

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads