Addai

From Wikipedia, the free encyclopedia

Addai
Remove ads

Addai, kwa Kiaramu ܐܕܝ,[1] ni mtakatifu anayeheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo, hasa wa Mashariki, ingawa hakuna makubaliano ya wanahistoria kuhusu maisha yake.

Thumb
Addai katika picha takatifu ya monasteri ya Mt. Katerina kwenye mlima Sinai, Misri.
Remove ads

Masimulizi juu yake

Kadiri ya mapokeo, hasa ya kitabu Mafundisho ya Addai, alikuwa Myahudi mzaliwa wa Edessa, wakati ule sehemu ya Syria, siku hizi nchini Uturuki.

Alipokwenda kuhiji Yerusalemu, alimsikiliza Yohane Mbatizaji na kubatizwa naye katika mto Yordani, akabaki Palestina.

Baadaye akawa mfuasi wa Yesu, akachaguliwa naye kati ya wanafunzi 70 kwenda kuhubiri wawiliwawili.

Baada ya ufufuko wa Yesu na Pentekoste ya mwaka uleule, Addai alianza kuhubiri Injili huko Mesopotamia, Syria na Persia.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Agosti, pamoja na mwanafunzi wake Mari.

Hata leo inatumika anafora yenye majina yao isiyo na simulizi la Karamu ya mwisho, tofauti na nyingine zote.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads