Utume wa Yesu
Marejeo From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Utume wa Yesu katika Injili, unaanza na ubatizo wake kwa mkono wa Yohane Mbatizaji katika mto Yordani na unakamilika katika mji mtakatifu wa Yerusalemu kwa kifo chake msalabani.[1]


Injili ya Luka (3:23) inasema Yesu Kristo alipoanza utume wake alikuwa "na umri wa miaka 30 hivi".[2]
Kwa kawaida wataalamu wa Biblia wanakadiria kwamba mwaka wa kubatizwa ulikuwa kati ya 27 na 29 BK na ule wa kuuawa kati ya 30 na 33.[3]
Awali Yesu, baada ya kubatizwa na kukaa siku 40 katika jangwa la Yudea, alifanya kazi ya kitume zaidi katika mkoa wa Galilaya, huko alikokulia,[4] akihubiri na kuponya, pamoja na kufukuza pepo wachafu.
Mbali ya hiyo miujiza yake, ni muhimu mwenendo wake wa kukaribiana na watu wa kila aina, bila ubaguzi: tendo lake la kushiriki karamu pamoja na wakosefu lilichukiza wengi, hasa kati ya madhehebu ya Mafarisayo waliokwepa watu hao. Kumbe kwa Yesu lilikuwa dokezo la kwamba Mungu anawaalika wote kutubu na kuingia raha ya ufalme wake.
Wakati huohuo aliita baadhi kumfuata kama wanafunzi katika safari zake. Kati yao aliteua mitume 12 kama mwanzo wa Kanisa lake.[1][5]Hao aliwaita mitume kwa sababu aliwapeleka kwanza kwa Waisraeli (Math 8) lakini baada ya kufufuka kwa mataifa yote pia (Math 28:16-20).[6][7]
Baada ya kifodini cha Yohane Mbatizaji, Yesu alijiandaa kwenda Yerusalemu kwa mara ya mwisho ili kukamilisha utume wake kwa kujitoa kafara alivyotabiriwa na Yohane: "Huyu ndiye mwanakondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu".[8][9]
Safari hiyo ya mwisho ilimchukua tena kwa muda karibu na mahali alipobatizwa.[10][11][12][13][14]
Utume wake wa mwisho mjini Yerusalemu ulianza na tukio la kuingia Yerusalemu kwa shangwe ya Wayahudi walioamini kwamba ndiye Masiya, hasa baada ya muujiza mkuu alioufanya, yaani kumfufua Lazaro wa Bethania kutoka kaburini siku ya nne baada ya kifo. Injili zinasimulia kirefu zaidi habari za hiyo wiki ya mwisho kutokana na umuhimu wake kama kilele cha yote.[15]
Remove ads
Ushahidi wa Petro
Mtume Petro alisimulia kifupi utume wa Yesu kama ifuatavyo (Mdo 10:34-43):
34 Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo; 35 bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye. 36 Neno lile alilowapelekea wana wa Israeli akihubiri habari njema ya amani kwa Yesu Kristo (ndiye Bwana wa wote), 37 jambo lile ninyi mmelijua, lililoenea katika Uyahudi wote likianzia Galilaya, baada ya ubatizo aliouhubiri Yohana; 38 habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye. 39 Nasi tu mashahidi wa mambo yote aliyoyatenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu; ambaye walimwua wakamtundika mtini. 40 Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu, akamjalia kudhihirika, 41 si kwa watu wote, bali kwa mashahidi waliokuwa wamekwisha kuchaguliwa na Mungu, ndio sisi, tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu. 42 Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na wafu. 43 Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.
Remove ads
Picha
- Wito wa Mathayo kadiri ya Vittore Carpaccio, 1502
- Wanafunzi wa kwanza wa Yesu na Uvuvi wa ajabu
- Kutuliza dhoruba
- Mawaidha kwa Mitume
- Wanafunzi Sabini
- Wajumbe wa Yohane Mbatizaji
- Flevit super illam (Alilia juu yake), kadiri ya Enrique Simonet, 1892.
- Utakaso wa Hekalu kadiri ya Giotto.
- Ole wenu Mafarisayo
- Yuda akipanga bei ya Yesu
- Maneno ya buriani
Remove ads
Tanbihi
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads