Mbuga za Taifa la Tanzania

Makala ya orodha ya Wikimedia From Wikipedia, the free encyclopedia

Mbuga za Taifa la Tanzania
Remove ads

Mbuga za Taifa za Tanzania[1] ni nyingi tena mbalimbali, zikishika karibu theluthi moja ya eneo lote la nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Thumb
Mahali pa mbuga za taifa nchini Tanzania.

Zinagawanyika kati ya:

  • Hifadhi za Taifa,
  • Hifadhi Teule,
  • Hifadhi ya Mawindo na
  • Mapori ya Akiba.

Hifadhi za taifa

Hii ni orodha ya Hifadhi za Taifa, ambazo ni 19:

Maelezo zaidi Hifadhi za Taifa, Kiingereza ...

Hakuna budi kuweka ulinzi mbugani kwani kuna majangili wanaoua ovyo wanyama kama vile tembo na kifaru: wanyama hao wanaweza kusaidia katika kuinua pato la taifa kupitia utalii.

Remove ads

Hifadhi za bahari na maeneo tengefu

Ni mpango wa kimataifa kuwa asilimia 10 ya maji ya bahari na maziwa yawe chini ya hifadhi, na Tanzania ina asilimia 4.5 tu ya hifadhi ambayo inahusisha hifadhi za bahari 3 na maeneo tengefu 15.

Hifadhi za bahari

Thumb
Hifadhi ya kisiwa cha Mbudya, Dar es Salaam.

Hifadhi ya Bahari ni eneo kubwa ambalo hata watu wanaishi ndani yake. Shughuli za eneo hilo husimamiwa na Mpango wa Usimamiaji ujulikanao kama General Management Plan, ambao maandalizi yake yanashirikisha wadau woteː wanaoishi ndani ya hifadhi, Halmashauri husika ambazo ziko ndani ya hifadhi, na wengineo wakiwa ni pamoja na wanasayansi. Yanafanyika makubaliano ya kuwa baadhi ya maeneo yatengwe kabisa ambapo hakuna uvuvi wowote utakaoruhusiwa, kutenga maeneo ya matumizi ya jumla ambapo uvuvi unaruhusiwa kwa wavuvi wa ndani na nje ya hifadhi na maeneo ya matumizi maalum ambayo pamoja na kwamba wavuvi wa ndani ya hifadhi wanaruhusiwa kuvua kwa kutumia zana maalumu zinazokubalika, wavuvi wa nje hawaruhusiwi kabisa kuvua katika maeneo hayo.

Maeneo tengefu

Thumb
Kisiwa cha Bongoyo

Maeneo tengefu ni maeneo madogomadogo ya visiwa ambayo yanazungukwa na matumbawe. Katika maeneo hayo watu hawaruhusiwi kuishi wala matumizi ya rasilimali hayaruhusiwi. Shughuli zinazoruhusiwa katika maeneo hayo ni zile zinazohusiana na utalii tu. Maeneo hayo ni pamoja na visiwa vya Bongoyo na Mbudya mjini Dar es Salaam ambapo ndani yake kitengo kimetengeneza njia vinjari (nature trails) kwa ajili ya watalii kupita.

Remove ads

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads