Mkoa wa Simiyu
kanda ya Ziwa, Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mkoa wa Simiyu ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Ulianzishwa rasmi Machi 2012 kwa kumega mkoa wa Shinyanga upande wa mashariki[1]. Eneo lake ni la km2 25,212. Unapakana na mikoa ya Mara upande wa kaskazini, Arusha upande wa mashariki, Shinyanga na Singida upande wa kusini, Mwanza upande wa magharibi. Ndani ya eneo lake kuna sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo imeorodheshwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia. Kadiri ya sensa ya mwaka 2022, mkoa una wakazi 2,140,497 [2]. Makao makuu yako Bariadi.

Remove ads
Wakazi
Kadiri ya sensa ya mwaka 2022, mkoa una wakazi 2,140,497 [4] kutoka 1,584,157 wa mwaka 2012, [5] walipokuwa wameongezeka 1.8% kwa mwaka katika miaka 2002-2012[5].
Msongamano wa watu ulikuwa 63 kwa kilomita mraba.[5]
Wilaya
Mkoa huo mpya una wilaya 6 zifuatazo: Bariadi Mjini, Bariadi, Busega, Maswa, Meatu, Itilima.
Majimbo ya bunge
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Bariadi : mbunge ni Andrew Chenge (CCM)
- Busega : mbunge ni Raphael Chegeni (CCM)
- Itilima : mbunge ni Njalu Silanga (CCM)
- Kisesa : mbunge ni Luhaga Mpina (CCM)
- Maswa Mashariki : mbunge ni Stanslaus Nyongo (CCM)
- Maswa Magharibi : mbunge ni Mashimba Ndaki (CCM)
- Meatu : mbunge ni Salum Khamis Salum (CCM)
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads