Mkoa wa Simiyu
kanda ya Ziwa, Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mkoa wa Simiyu ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania, wenye postikodi namba 39000 [1]. Ulianzishwa rasmi Machi 2012 kwa kumega mkoa wa Shinyanga upande wa mashariki[2]. Makao makuu yako Bariadi.

Wakazi
Kadiri ya sensa ya mwaka 2022, mkoa una wakazi 2,140,497 [3] kutoka 1,584,157 wa mwaka 2012, [4] walipokuwa wameongezeka 1.8% kwa mwaka katika miaka 2002-2012[4].
Msongamano wa watu ulikuwa 63 kwa kilomita mraba.[4]
Wilaya
Mkoa huo mpya una wilaya 6 zifuatazo: Bariadi Mjini, Bariadi, Busega, Maswa, Meatu, Itilima.
Majimbo ya bunge
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Bariadi : mbunge ni Andrew Chenge (CCM)
- Busega : mbunge ni Raphael Chegeni (CCM)
- Itilima : mbunge ni Njalu Silanga (CCM)
- Kisesa : mbunge ni Luhaga Mpina (CCM)
- Maswa Mashariki : mbunge ni Stanslaus Nyongo (CCM)
- Maswa Magharibi : mbunge ni Mashimba Ndaki (CCM)
- Meatu : mbunge ni Salum Khamis Salum (CCM)
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads